.

.

Jumatano, 14 Desemba 2016

MAHUSIANO CUP YAHAMASISHA MAMIA KUJITOKEZA KUPIMA VVU WAKATI WA MCHEZO WAFAINALI

Mgeni rasmi katika fainali za Mahusiano Cup, katibu tawala wa wilaya ya Kahama, Timoth Ndanya (Katikati) akipokea maelezo kutoka kwa mwamuzi wa mchezo wa fainali kati ya timu za kata ya Mhungula.Kushoto ni Kaimu Meneja Mkuu wa Mgodi wa Buzwagi George Mkanza, wengine katika picha ni Solomon Rwangabwoba- Meneja Ufanisi na raslimali watu (katikati ya mwamuzi na katibu tawala) wengine ni mwenyekiti wa KDFA Bwana Ibrahim Khan na Bwana Magesa Magesa Afisa Mawasiliano Mgodi wa Buzwagi.
Katibu tawala Wilaya ya Kahama Timoth Ndanya akisalimiana na wachezaji wa timu ya Kahama Mji.
Katibu tawala Wilaya ya Kahama Timoth Ndanya akisalimiana na wachezaji wa timu ya kata ya Mhungula.
Kaimu Meneja Mkuu wa Mgodi wa Buzwagi George Mkanza akisalimiana na wachezaji wa timu ya kata ya Mhungula, nyuma yake ni Meneja Ufanisi na raslimali watu wa Mgodi wa Buzwagi,Solomon Rwangabwoba.
Mgeni rasmi Katibu tawala wa wilaya ya Kahama,Timoth Ndanya akisalimiana na wachezaji wa timu ya netball ya kata ya  Zongomela.
Mgeni rasmiKatibu tawala wa wilaya ya Kahama, Timoth Ndanyaakisalimiana na wachezaji wa timu ya netball ya kata ya Kahama Mjini.