.

.

Alhamisi, 22 Septemba 2016

TFF imetangaza kusitisha matumizi ya uwanja wa Uhuru kwa wiki tatu



Siku moja imepita toka waziri wa habari, sanaa, utamaduni na michezo waziri
Nape Moses Nnauye aweke wazi kuwa Simba na vilabu vingine vinavyolalamikia
uwanja waUhuru kuwa sio salama kwa afya za wachezaji, na kuomba kutumia
Taifa kuwa waiombe bodi ya Ligi kwani ndio wanaopanga michezo ichezwe
uwanja gani.
Leo Septemba 21 2016 afisa habari wa shirikisho la soka Tanzania TFF
Alfred Lucasameweka wazi maamuzi ya TFF
“Baada ya malalamiko ya vilabu vya Dar es Salaam kuhusu kuutumia uwanja
wa Uhuru, TFF inaufunga uwanja huo na mechi kuzihamishia Taifa
kutokana na  kugundua kuwa plastic zilizopo katika pitch ya Uhuru
zimekauka hivyo zinawaumiza wachezaji, ukarabati tunategemea uchukue
wiki mbili hadi tatu”